Dk Nangale: Tuiweke nyumba yetu katika hali nzuri kabla ya kukaribisha wageni
MIONGONI mwa mambo ambayo yametiliwa kasi katika mwaka uliopita wa 2006 ni mchakato wa haraka wa kuelekea Shirikisho la Afrika Mashariki (fast trucking).
Wiki iliyopita mbunge wa Afrika Mashariki Dk. George Nangale alielezea umuhimu wa kuingia katika Shirikisho la Afrika Mashariki na makubakubaliano ya mchakato wa kuelekea kwenye shirikisho. Kuhusu mpango kasi kuelekea Shirikisho, Dk Nangale anasema kuwa yeye haoni sababu za kuufanya mchakato huo polepole sana wala haraka sana, unaweza ukafikiwa kwa taratibu zake za kawaida kama ilivyokubaliwa awali. Hii ni sehemu ya pili ya mahojiano baina ya mwandishi HAWRA SHAMTE na Dk Nangale kuhusu mchakato wa Shirikisho la Afrika Mashariki.
Swali: Kwanini haraka ya kwenda kwenye Shirikisho?
Jibu: Miaka miwili iliyopita Rais Benjamin Mkapa, Rais Museveni na Rais Mwai Kibaki walikutana Nairobi katika mkutano wa dharura. Kulikuwa kuna ajenda kwamba kwani ni lazima awamu zilizopangwa kufikia Ushirikiano ni lazima ziende kwa utaratibu huo? Haiwezekani kuziharakisha? Wakaunda Tume kujadili suala hilo, wakaunda Tume ya Wako ambayo ilizunguka na kukutana na wadau mablimbali, wabunge, wananchi, wafanyabiashara na ilifanya kazi kwa muda wa miezi sita. Ilipotoa ripoti yake, ile Tume ikasema kwamba wananchi wa Afrika Mashariki wako tayari kuharakisha muungano wa Afrika Mashariki na ikatengeneza ratiba kwamba ifikapo mwaka 2010 tuwe tumeshafikia hatua fulani, 2012 tuwe na kura ya maoni na 2013 hizi nchi ziwe zimeshaungana kisiasa. Hiyo haina maana kwamba hatua za kufikia Ushirikiano wa kisiasa zitafutwa, la hasha, bali awamu zote zitaharakishwa ama zitatekelezwa kwa pamoja.
Ripoti ile ikapelekwa kwenye mabunge ikajadiliwa. Bunge la Uganda waliizungumza, Bunge la Kenya wabunge walisomewa tu lakini hawakuizungumza rasmi, Bunge la Tanzania haikuizunguza rasmi ripoti ile. Katika Bunge la Tanzania ripoti ile ilizungumzwa kwenye semina ya wabunge, wabunge wengi waliikataa ripoti ile, lakini haikuzungumzwa katika kikao rasmi cha Bunge.
Katika Bunge la Afrika Mashariki ripoti ile ilipelekwa ingawa haikujadiliwa rasmi. Wakuu wa nchi walipopata ile ripoti wakakubaliana kuunda kamati za kuendesha mijadala, ili wananchi wapate nafasi ya kutoa maoni. Kila nchi ikaunda kamati, kamati hizo zimepewa miezi minane ya kukusanya maoni ya wananchi. Itakapofika Mei mwakani wanapaswa kuiwasilisha ripoti yao kwenye Baraza la mawaziri.
Swali ni je Kamati ya kukusanya maoni kwa upande wa Tanzania tayari imeshaanza kazi ya kukusanya maoni? Imesalia miezi minne tu Kamati hiyo inapaswa iwasilishe ripoti yake.
Swali: Je kuna changamoto gani zinazoikabili Jumuiya?
Jibu: Wasiwasi wangu mkubwa ni kuwa Jumuiya yetu watu hawaifahamu vizuri hivyo Serikali na wadau wote wa Afrika Mashariki wanapaswa wafanye kazi kubwa ya kuwaelimisha Watanzania kuhusu dhana nzima ya Afrika Mashariki.
Nia kubwa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kuinua hali za wananchi wa Afrika Mashariki. Kwa viwango vya dunia, wananchi wa Afrika Mashariki ni masikini sana na tunataka tupande na njia mojawapo ya kutuwezesha kupanda ni kuwa na masoko ya pamoja, kufanya biashara ya pamoja, kuzalisha kwa wingi, pamoja, msingi wa kuwa pamoja na msingi unaoeleweka kwa ajili ya maendeleo ya watu. Pia tunataka eneo letu liwe la kiushindani duniani, sasa hivi tuna mikataba mikubwa iankuja kutoka marekani wka mfano ya pamba, AGOA na kadhalika lakini tunashindwa kuitekeleza kama nchi mojamoja kwa sababu ya ule uwezo wetu na udogo wetu, kwa hivyo tukiunganisha nguvu pamoja, tunaweza tukanufaika zaidi.
Swali: Je ikiwa tutakapokuwa Shirikisho, ushiriki wetu katika jumuiya nyingine kama vile SADC na COMESA unakuwaje?
Jibu: Kuna misingi inayofuatwa duniani katika masuala ya mashirikiano. Mathalan haiwezekani kuwa katika Ushuru wa pamoja wa Forodha katika jumuiya zaidi ya moja. Hiyo ndiyo misingi ya kibiashara duniani iliyowekwa na World Trade Organization (WTO). Kwa hivyo ushirikiano wetu na jumuiya nyingine hauzuiliwi. Isipokuwa unaweza ukawa mdogo kwa mfano hatuwezi tukafanya ushirikano na SADC ambao unatuingiza katika Umoja wa Forodha wa SADC kama tayari tuko katika Umoja wa Forodha wa EAC. Sisi kama Afrika Mashariki tunaweza tukazingumza na wenzetu tukawaambia kwamba SADC ni muhimu kwa Afrika Mashariki, siyo muhimu kwa Tanzania peke yake, kwa hiyo tutafute namna ya kushirikiana na SADC kama Afrika Mashariki. Vivyo hivyo Kenya na Uganda nao wanaweza wakatushawishi kwamba COMESA ni muhimu siyo kwa Kenya na Uganda peke yake hata kwa Tanzania, hivyo tushauriane tutawezaje kushirikiana pamoja ndani ya COMESA. Kwa mfano kama sote tulio katika ushirikiano tutakubaliana tuingie SADC au COMESA kama Afrika Mashariki, haizuliwi.
Ninachosisitiza ni kwamba haya mambo ni mchakato, hakuna sababu ya kwenda haraka sana na hakuna sababu ya kwenda pole pole sana. Kusema kwamba tuingie katika Shirikisho 2013 ni pendekezo tu, kama Watanzania, Wakenya na Waganda wanataka iwe hivyo itakuwa hivyo lakini kama wananchi wa Afrika Mashariki hawataki iwe hivyo haiwezi kuwa hivyo.
Swali: Je nini uelewa wa wananchi wa Afrika Mashariki kuhusu Shirikisho?
Jibu: Wananchi wa Afrika Mashariki wanaelewa umuhimu wa kuingia katika Shirikisho na wanaelewa umuhimu wa kuwa na jumuiya yenye nguvu. Tatizo linakuja kwamba namna gani tufikie hapo? Bado kuna tofauti nyingi za kisheria na kisera katika nchi zetu. Kwa hiyo kazi kubwa ambayo nchi zinatakiwa ziifanye ni kuainisha sera kwa sababu sera zetu bado ziko tofauti sana. Tukiweza kuainisha sera zetu kwa haraka iwezekanavyo, ambao nadhani ndio msisitizo ungekuwapo hapo kwa sasa hivi, kwa kufanya hivyo kuungana itakuwa ni rahisi zaidi.
Wananchi wengi hawana hofu, hasa wale wa kawaida, isipokuwa ukienda kwa wasomi na wanasiasa wengi wanasita kwa sababu wanaangalia maslahi yao zaidi, je tukiungana nafasi zetu kama wanasiasa zitakuwaje? Lakini wananchi wa kawaida kama kweli jumuiya itawanufaisha, wao wako tayari. Hofu kubwa ya wananchi mathalan wa Tanzania yako katika ajira na ardhi.
Swali: Kwanini hofu ya Watanzania iko katika ajira?
Jibu: Mfumo wetu wa kielimu tuliokuwa nao toka mwanzo hautupi nafasi kubwa ya kuweza kuingia katika ushindani wa kiajira. Lakini hata hivyo mara nyingine hofu hayo haina mashiko sana, kwa sababu kuna Watanzania wengi wanaofanya kazi katika nchi mbalimbali, ukienda Lesotho, ukienda Botswana, Watanzania ndio wametamalaki katika taasisi za kielimu, kwa hiyo unaweza ukakuta watu wa Botswana wanawalalamikia Watanzania kama sisi tunavyowalalamikia Wakenya.
Lakini hatimaye watu wa Botswana wananufaika sana kwa sababu wanafunza vijana wao, baada ya miaka 20 au 30 ijayo watakuwa wameshafikia kiwango cha kujitosheleza na pengine hawatawahitaji tena Watanzania. Kwa hiyo hata Wakenya wakifurika Tanzania sasa hivi, hawatafurika milele, watakuwapo kwa muda fulani lakini baadaye watatuwezesha nasisi kujiwezesha kufikia kiwango hicho na kuboresha mifumo yetu.
Nadhani tusihofu sana kwa hilo, kwa sababu ni suala la wakati tu, Watanzania wako wengi, wanazaliana kila siku, watu milioni 30 kama ukimwi utaweza kudhibitiwa, nadhani tutafikia mahala tutaweza kushindana. Labda suala la msingi ni kwamba tupange vizuri sera zetu za elimu, hicho ndicho kitu cha msingi, lakini kuwa na hofu kwamba Wakenya watadhibiti ajira zetu si hofu ya msingi sana kwani hakuna mtu anayetaka kuhama Kenya kuja kuishi Tanzania, hata hapa Tanzania nani anapenda kutoka vijijini kuja kuishi mijini? Ni kwa sababu kuna tofauti, kama hakuna tofauti mtu anapenda kukaa alipo. Watu wengi sana wanaogopa kuhama, hata Wakenya nao wanaogopa kuhama, siyo kweli kama tukifungua milango leo, Wakenya watajaa. Watakuja wachache lakini hatimaye watarudi kwao.
Swali: Kwanini hofu iwepo katika masuala ya ardhi?
Nadhani tatizo lililopo Tanzania ni kuwa bado hatujajiweka sawa katika suala la ardhi. Ni vizuri tujiweke sawa na taratibu za kumiliki ardhi yetu. Hawa wageni wakija hawaibebi ardhi, wakiichukua wanakuja kuzalisha, kwanini tuwazuie? Tanzania kuna mapori tele, tuwaruhusu wayaendeleze ila tuweke vizuri sera zetu za kumiliki ardhi.
Mimi nadhani tunapaswa kuiweka nyumba yetu katika hali nzuri, (lets make our house in order) halafu tuwakaribishe wenzetu. Hatuna sababu kubwa ya kuhofia ardhi, kwa sababu zaidi ya asilimia 50 ya ardhi ya Tanzania iko katika hifadhi.
Swali: Dk. Nangale wewe ni mtunzi wa kitabu cha Politics of Partneship, kitu gani kilikusukuma kuandika kitabu hicho?
Jibu: Azma yangu ilikuwa ni kuweka wazi misingi ya ushirikiano. Nimejaribu kueleza mambo mengi ndani yake, nimejaribu kueleza jinsi gani taasisi na watu waliomo ndani ya taasisi, mahusiano yao yanaweza yakajenga au yakabomoa ushirikiano. Ushirikiano ni lazima uwe ni kitu cha kutoa na kuchukua. Dhana ya uhusiano ni ya muhimu sana katika kudumisha ushirikiano. Katika Afrika Mashariki tunayo bahati kwamba tuna uhusiano wa kihistoria, kwa sababu ukiangalia uhusiano wetu wa Afrika Mashariki kwa kweli ulikuzwa na mkoloni, mkoloni alijaribu kuziweka hizi nchi pamoja kwa manufaa yake, lakini ametutengeneza lugha ya Kiswahili kwa sababu lugha ya Kiswahili ni zao la mkoloni. Alijaribu kufanya mahusiano na watu wa Afrika Mashariki kwa kutumia ile lugha, kwa hiyo alichukua lugha yake, akachukua lugha za Waarabu, akachukua lugha za kibantu akaunda lugha maalum ya Kiswahili ambayo sasa hivi inatuunganisha sisi Watanzania na watu wa Afrika Mashariki.
Kama utakisoma kitabu hicho utagundua kwamba nazungumza kuhusu ushirikiano kwa filosofia zaidi, kwani ukweli ni kwamba tunaungana lakini wakati huo huo hatuungani. Kuna masuala ambayo tunajaribu kuunganisha yale ambayo tunafanana na tuna masuala ambayo kwa kweli hatuwezi tukayaunganisha kwa sababu za kihistoria na tofauti zetu. Ili muungano wetu uwezo kufanikiwa, lazima tukubaliane na tofauti zetu, kwamba tofauti zetu lazima zitaendelea kuwapo lakini kuungana tutaendelea kuungana. Wakenya watabaki Wakenya, Watanzania watabaki Watanzania, Waganda watabaki Waganda na kadhalika.
Swali: Je Umoja wa Afrika Mashariki utakuwa sawa na ule Umoja wa Ulaya (EU)?
Jibu: Umoja wa Ulaya si kigezo chetu, Ushirikiano wetu ni wa kipekee. Nchi za Ulaya hazijaungana mpaka leo, wamekubaliana mambo fulani fulani tu, katika masuala ya kijamii yaliyiozungumzwa katika mkataba wa Mostrich unaozungumzia masuala ya jamii, Uingereza na Denmark wamejitoa, Sarafu ya Pamoja, Uingereza na Denmark wamejitoa. Umoja wa Ulaya unashikiliwa na Ufaransa na Ujerumani lakini leo Ujerumani ikijitoa kwenye Euro, Euro itaanguka. Kwa hivyo sisi Afrika Mashariki tuna azma kubwa zaidi kuliko Umoja wa Ulaya, sisi sasa hivi tunafikiria kuunda ‘Supra State’ taifa la Afrika Mashariki, Ulaya hawajafikia hiyo hatua, wako mbali sana kufikia Taifa la Ulaya, wao wameungana katika mambo ya Ushuru wa Forodha na Soko la Pamoja lakini katika Shirikisho la kisiasa hawajafikia.
Swali: Je tutaweza kukabiliana na changamoto za Shirikisho ama Muungano?
Jibu: Watanzania tunao uzoefu wa miaka zaidi 40 ya Muungano, kwa hivyo Watanzania ni walimu wazuri sana kwa wenzetu kwamba Muungano au Shirikisho si kitu rahisi sana, majadiliano ya mara kwa mara na ya muda mrefu yanahitajika, ni kitu cha kujadiliana kwa miaka mingi, yaweza hata kufikia miaka 50 mnajadiliana tu kabla hamjafikia pale mnapopataka ama mliporidhiana.
Friday, January 26, 2007
Monday, January 22, 2007
Shirikisho la Afrika Mashariki
Hi Comrades!
Leo nawaletea makala niliyoitoa mwishoni mwa Desemba kuhusu East Africa Community/Federation. Hii ni sehemu ya kwanza, I hope it will be educative.
Karibuni...
Dk Nangale: Mchakato wa Shirikisho wahitaji mijadala ya kina na muda zaidi
MIONGONI mwa mambo ambayo yameshika kasi wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne ambayo Desemba 21 mwaka huu ilitimiza mwaka mmjoa tokea iingie madarakani ni suala la kuharakisha ushirikiano wa kisiasa wa Afrika Mashariki (Shirikisho). Suala ambalo bado halijapata udadavuzi wa kina ni kuhusu kwanini tuwe na haraka ya kufikia Shirikisho? Imepangwa kuwa ifikapo mwaka 2013, nchi za Afrika Mashariki ziungane na kuwa nchi moja katika mfumo wa Shirikisho kwa maana ya kuwa pamoja na kwamba kila nchi itakuwa na Rais wake, Serikali yake, Bunge lake na Mahakama zake, lakini nchi hizo ziunganishwe katika mwamvuli mmoja wa Afrika Mashariki ambao utakuwa na Rais wa Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika Mashariki sambamba na kulifanya eneo hilo kuwa ni eneo moja la kibiashara linalotambulika kimataifa. Katika makala hii, mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na mbunge mkongwe wa Bunge la Afrika mashariki na ambaye pia ni Mwenyektii wa kamati ya Mawasiliano Biashara na Vitega uchumi katika Bunge la Afrika Mashariki, DK GEORGE NANGALE ambaye analieleza kwa kina chimbuko la kuwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki, muundo wake, taratibu zake na makubaliano yaliyofikiwa. Kadhalika Dk. Nangale anajibu swali la kwanini kuharakisha Shirikisho?
“Tulipoanzisha upya Jumuiya ya Afrika Mashariki, miaka 10 iliyopita, tutakumbuka kwamba ilitokana na azimio lililotolewa baada ya kuvunjika ile ya zamani. Sasa wakati wanajaribu kukusanya na kugawana zile rasilimali zilizokuwapo wakaona kwamba siyo kitu cha busara kufuta kabisa kila kitu. Kwa hiyo kuna taasisi zilibaki, kama vile East African Development Bank na taasisi nyingine kama zile za utafiti. Lakini vilevile yakatokea mawazo kwamba siku zijazo ni vizuri tuangalie upya namna gani tutaweza kushirikiana, kwa hiyo wale marais waliokuwapo wakati ule, Rais Daniel Arap Moi, Rais Ali Hassan Mwinyi na Rais Yoweri Museveni waliangalia jinsi ya kuifufua Jumuiya ya Afrika mashariki. Walipokubaliana hivyo, mwaka 1996 wakasema kwamba wananchi waanze kujadili, kuona waunde jumuiya ya aina gani. Yakaanza majadiliano katika nchi hizo tatu, majadiliano yale yalishirikisha Serikali na Wadau, yalichukua miaka minne,” anasema Dk.George Nangale.
“Kwa kuwa kulikuwa na mawazo kwamba pengine ni vizuri kuunda jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Mashariki, wadau kama wafanyabiashara, Jumuiya za kijamii, wasomi na Serikali walianza kujadili suala hilo. Kwa hiyo kulikuwa kuna mjadala kaunzia 1996 mpaka 1999. Ilipofika Novemba 1999, wataalam wetu, wanasheria wakuu na wabunge walipata nafasi ya kulijadili suala hilo kwa undani kwamba je tunaanzisha jumuiya ya aina gani?
“Novemba 30 , 1999 ukasainiwa mkataba (Treaty for the Establishment of East African Community) viongozi wakakubaliana kuwa utaanza rasmi kazi zake Julai mosi 2000. mkataba ule umejikita katika mambo makuu matano, kwanza muundo, je tutakuwa na muundo wa aina gani?
Muundo wa Jumuiya:
“Makubaliano yakawa kwamba Jumuiya ya Afrika Mashariki itakuwa na asasi (organs) mbalimbali ambazo zitasaidia kusukuma mbele azma ya jumuiya yenyewe. Hivyo tukakubaliana kwamba kutakuwa na Sekretarieti na Arusha itakuwa ndiyo makao makuu ya jumuiya. Sekretarieti itasimamia shughuli za kila siku za jumuiya, pia tukakubaliana kuwa kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo kazi yake itakuwa ni kusimamia sera. Ilionekana kwamba kazi kubwa ya Jumuiya ni kuainisha na kuziweka sawa sera zetu kwa sababu tutakuwa na sera zinazotofautiana,” anasema Dk. Nangale.
“Asasi ya tatu ni Bunge, kwamba tutakuwa na Bunge la Afrika Mashariki ambalo kazi yake kubwa itakuwa ni kutunga sheria ambazo zitakuwa zinaongoza masuala yote ambayo tutakubalina wkamba tutayafanya kwa pamoja, siyo kutunga sheria zote ila kuhusu yale mambo tuliyokubaliana kwa wakati huo.
“Asasi nyingine ni Mahakama ya Afrika Mashariki. Mahakama hii si mahakama ya rufaa, ni mahakama ambayo kimsingi inatafsiri uhusiano wetu kwa maana ya kutafsiri katiba. Kama kuna tofauti zozote za utekelezaji wa katiba au masuala tuliyokubaliana, mahakama itakuwa inaingilia kati kutoa ufafanuzi na kutoa mapendekezo kwamba hili limefanyika sawa au siyo sawa.
“Asasi nyingine ni ‘Summit,’ Wakuu wa Nchi. Hawa watakutana katika Baraza lao la Wakuu wa Nchi, hawa ndio wasimamizi wakuu wa shughuli zote za Jumuiya. Kazi yao moja ni kuridhia yale tuliyoyapitisha bungeni na ni lazima marais wote waridhie ndipo suala hilo litakapopita. Kwa hiyo Summit ndiyo asasi ya juu zaidi kuliko asasi zote za Afrika Mashariki.”
Misingi ya Ushirikiano (The Principle of Cooperation):
Shabaha yetu ilikuwa ni kutoka kwenye ushirikiano mdogo (Cooperation) kwenda kwenye mahusiano makubwa (Integration). Ili tufanye hivyo kuna misingi mitatu tuliyokubaliana.
Msingi wa kwanza ni ‘Principle of Subsidiarity’;
Ni msingi ambao tunakubaliana kwamba katika ushirikiano wetu hatuwezi tukashirikiana katika kila kitu, kuna baadhi ya mambo tutashirikiana na baadhi ya mambo hatuwezi kushirikiana. Kwa hiyo tutashirikiana katika masuala fulani fulani ambayo tunadhani kwamba tunaweza tukashirikiana kwa ridhaa ya nchi zenyewe.
Msingi wa pili ni ‘Principle of Variable Geometry’;
Ni msingi ambao unatambua kwamba nchi zetu ziko tofauti, kiuchumi, kisiasa, kimuundo na masuala mengi ambayo yako tofauti, kwa hiyo tunakubali kwamba asasi mbalimbali zilizomo ndani ya hizi nchi zitashirikiana kwa sasi zao na utaratibu wao. Kwa mfano jumuiya za wakulima labda zinakwenda taratibu kuliko zile za wafanyabiashara, kwa hivyo zitakwenda kwa kasi tofauti na misingi tofauti.
Msingi wa tatu ni “Principle of Assemetry’
Msingi huu unasema kwamba iwapo A ni sawa na B siyo lazima B iwe sawa na A. Maana yake ni kwamba kwa kutambua tofauti zetu siyo lazima nchi moja inavyoifanyia nchi nyingine kwamba ni lazima nchi hiyo nayo ifanye hivyo hivyo. Kwa mfano msingi huu umefanyiwa kati katika ushirikiano wa forodha, kwamba Tanzania itapeleka bidhaa zake Kenya bila ushuru kwa sasa hivi, wakati Kenya tutawatoza ushuru ili kujipa muda wa kujirekebisha kwa muda wa miaka mitano.
Namna ya kufikia maamuzi:
“Tulikubaliana katika Afrika Mashariki kwamba makubaliano yote yatafikiwa kwa pamoja. Kama limekuja jambo ambalo linataka maamuzi, ni lazima nyote mukubali, yaani nchi zote tatu zikubali. Hivyo tulikubaliana kwamba maamuzi yote ya Afrika Mashariki yatafanywa kwa ‘consesus’ kwa maana ya kwamba, Baraza la Mawaziri likikutana, Wakuu wa nchi wakikutana, kama mmoja atatofautiana na wenzake ina maana kwamba hilo suala litaendelea kujadiliwa, kwa hiyo majadiliano yataendelea mpaka wote wakubaliane, kwa hiyo ukisikia maamuzi yametolewa ya Afrika Mashariki ujue kwamba wote wamekubaliana, hakuna suala la kura bali makubaliano ya pamoja.
Awamu za utekelezaji wa makubaliano:
Tulikubalina kuhusu mahusiano yetu yaendeje, tulikubaliana kwamba tutakwenda hatua kwa hatua. Tulikubaliana kuwa kitu cha kwanza tutakachoanza nacho ni umoja wa ushuru wa forodha (Customs Union). Kwa sababu ilionekana kwamba uhusiano wetu mkubwa ambao ni lazima tuuimarishe ni ule wa kibiashara, ili kuwapa watu wetu masoko na kuinua maisha yao kupitia biashara.
Kwa hivyo tuliamua tuwe na awamu za mashirikiano, tukianzia na Umoja wa Ushuru wa Forodha. Suala la ushuru wa Forodha lilianza kujadiliwa tokea mwaka 1999 hadi 2004, protokali ikasainiwa Machi, 2004 na Bunge tukapitisha sheria ya Ushuru wa Forodha Desemba 2004 na ikaanza kutumika Januari 2005.
Awamu ya pili ni kuanzisha Soko la Pamoja (Common Market), majadiliano yake yameanza Julai mwaka huu na yataendelea mpaka 2008. Soko la pamoja linajumuisha pia masuala ya uhamiaji (free movement of people), masuala ya ajira, masuala ya kufanya biashara kwa pamoja yaani eneo moja la kibiashara duniani (East Africa is a single destination), kuwa na sheria zinazofanana, kuwa na sera zinazofanana hususan zile za kazi, kwamba tukiwa na sheria na sera zinazofanana za kazi, watu wetu wanaweza wakafanya kazi katika hizi nchi bila matatizo, tuwe na pasi za kusafiria za Afrika Mashariki na pia tuwe na vitambulisho.
Awamu ya tatu ni kuwa na Sarafu ya Pamoja (Single Currency/Monetary Union)
Majadiliano yalipangwa yaanze mwaka 2009 hadi 2011, hapo ndipo tuwe na Sarafu moja. Mwisho kabisa, baada ya kupitia awamu zote hizo ndipo tutakwenda kwenye Ushirikiano wa Kisiasa (Political Federation).
Mkataba uliposainiwa mwaka 1999 kulikuwa kuna makubaliano kwamba Afrika Mashariki itakwenda kwa awamu mpaka kufikia Federation, haikupangwa ratiba ya Federation kwa wakati huo, tulikubaliana kwamba tukimaliza awamu moja tutakwenda nyingine. Kwa mfano Ushuru wa Pamoja wa Forodha ilikuwa ni awamu ambayo ilipaswa kufanyiwa kazi kwa miaka mitano toka 2005 hadi 2010. Halafu majadiliano ya Soko la Pamoja yanaanza, na labda itaanza kufanya kazi mwaka 2009 hadi miaka mitano, baada ya hapo Sarafu ya Pamoja, majadiliano yanaweza yakaanza mapema lakini utekelezaji wake ukafanywa baadaye. Baada ya hapo ndio tuingie katika Shirikisho la Kisiasa.
Jumuiya ya watu
Makubaliano yaliyofikiwa mwaka 1999 katika kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki tulikubaliana kuwa tuunde jumuiya ya watu. Jumuiya ya mwanzo iliyovunjika ilikuwa ni ya Serikali (more inter-governmental). Sasa hii tunataka iwe ya watu (people centered), kwa hiyo watu washirikiane katika hatua mbalimbali na asasi mbalimbali. Pamoja na kuwa Serikali ni wadau lakini hata sisi wananchi pia ni wadau. Kwa hivyo hata sekta binafsi na asasi za kijamii zitapewa nafasi katika Jumuiya hii mpya ya Afrika Mashariki.
Kwanini haraka ya kwenda kwenye ushirikiano wa kisiasa?
“Miaka miwili iliyopita Rais Benjamin Mkapa, Rais Museveni na Rais Mwai Kibaki walikutana Nairobi katika mkutano wa dharura. Kulikuwa kuna ajenda kwamba kwani ni lazima awamu zilizopangwa kufikia Ushirikiano ni lazima ziende kwa utaratibu huo? Haiwezekani kuziharakisha? Wakaunda Tume kujadili suala hilo, wakaunda Tume ya Wako ambayo ilizunguka na kukutana na wadau mablimbali, wabunge, wananchi, wafanyabiashara na ilifanya kazi kwa muda wa miezi sita. Ilipotoa ripoti yake, ile Tume ikasema kwamba wananchi wa Afrika Mashariki wako tayari kuharakisha muungano wa Afrika Mashariki na ikatengeneza ratiba kwamba ifikapo mwaka 2010 tuwe tumeshafikia hatua fulani, 2012 tuwe na kura ya maoni na 2013 hizi nchi ziwe zimeshaungana kisiasa,” anasema Dk. Nangale.
“Hiyo haina maana kwamba hatua za kufikia Ushirikiano wa kisiasa zitafutwa, la hasha, bali awamu zote zitaharakishwa ama zitatekelezwa kwa pamoja.
Ripoti ile ikapelekwa kwenye mabunge ikajadiliwa. Bunge la Uganda waliizungumza, Bunge la Kenya wabunge walisomewa tu lakini hawakuizungumza rasmi, Bunge la Tanzania haikuizunguza rasmi ripoti ile. Katika Bunge la Tanzania ripoti ile ilizungumzwa kwenye semina ya wabunge, wabunge wengi waliikataa ripoti ile, lakini haikuzungumzwa katika kikao rasmi cha Bunge.
Katika Bunge la Afrika Mashariki ripoti ile ilipelekwa ingawa haikujadiliwa rasmi. Wakuu wa nchi walipopata ile ripoti wakakubaliana kuunda kamati za kuendesha mijadala, ili wananchi wapate nafasi ya kutoa maoni. Kila nchi ikaunda kamati, kamati hizo zimepewa miezi minane ya kukusanya maoni ya wananchi. Itakapofika Mei mwakani wanapaswa kuiwasilisha ripoti yao kwenye Baraza la mawaziri.
Lakini cha ajabu ni kwamba kwa upande wa Tanzania ndio kwanza inajiweka sawa katika kazi ya kukusanya maoni? Imesalia miezi minne tu Kamati hiyo inapaswa iwasilishe ripoti yake.
Leo nawaletea makala niliyoitoa mwishoni mwa Desemba kuhusu East Africa Community/Federation. Hii ni sehemu ya kwanza, I hope it will be educative.
Karibuni...
Dk Nangale: Mchakato wa Shirikisho wahitaji mijadala ya kina na muda zaidi
MIONGONI mwa mambo ambayo yameshika kasi wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne ambayo Desemba 21 mwaka huu ilitimiza mwaka mmjoa tokea iingie madarakani ni suala la kuharakisha ushirikiano wa kisiasa wa Afrika Mashariki (Shirikisho). Suala ambalo bado halijapata udadavuzi wa kina ni kuhusu kwanini tuwe na haraka ya kufikia Shirikisho? Imepangwa kuwa ifikapo mwaka 2013, nchi za Afrika Mashariki ziungane na kuwa nchi moja katika mfumo wa Shirikisho kwa maana ya kuwa pamoja na kwamba kila nchi itakuwa na Rais wake, Serikali yake, Bunge lake na Mahakama zake, lakini nchi hizo ziunganishwe katika mwamvuli mmoja wa Afrika Mashariki ambao utakuwa na Rais wa Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika Mashariki sambamba na kulifanya eneo hilo kuwa ni eneo moja la kibiashara linalotambulika kimataifa. Katika makala hii, mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na mbunge mkongwe wa Bunge la Afrika mashariki na ambaye pia ni Mwenyektii wa kamati ya Mawasiliano Biashara na Vitega uchumi katika Bunge la Afrika Mashariki, DK GEORGE NANGALE ambaye analieleza kwa kina chimbuko la kuwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki, muundo wake, taratibu zake na makubaliano yaliyofikiwa. Kadhalika Dk. Nangale anajibu swali la kwanini kuharakisha Shirikisho?
“Tulipoanzisha upya Jumuiya ya Afrika Mashariki, miaka 10 iliyopita, tutakumbuka kwamba ilitokana na azimio lililotolewa baada ya kuvunjika ile ya zamani. Sasa wakati wanajaribu kukusanya na kugawana zile rasilimali zilizokuwapo wakaona kwamba siyo kitu cha busara kufuta kabisa kila kitu. Kwa hiyo kuna taasisi zilibaki, kama vile East African Development Bank na taasisi nyingine kama zile za utafiti. Lakini vilevile yakatokea mawazo kwamba siku zijazo ni vizuri tuangalie upya namna gani tutaweza kushirikiana, kwa hiyo wale marais waliokuwapo wakati ule, Rais Daniel Arap Moi, Rais Ali Hassan Mwinyi na Rais Yoweri Museveni waliangalia jinsi ya kuifufua Jumuiya ya Afrika mashariki. Walipokubaliana hivyo, mwaka 1996 wakasema kwamba wananchi waanze kujadili, kuona waunde jumuiya ya aina gani. Yakaanza majadiliano katika nchi hizo tatu, majadiliano yale yalishirikisha Serikali na Wadau, yalichukua miaka minne,” anasema Dk.George Nangale.
“Kwa kuwa kulikuwa na mawazo kwamba pengine ni vizuri kuunda jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Mashariki, wadau kama wafanyabiashara, Jumuiya za kijamii, wasomi na Serikali walianza kujadili suala hilo. Kwa hiyo kulikuwa kuna mjadala kaunzia 1996 mpaka 1999. Ilipofika Novemba 1999, wataalam wetu, wanasheria wakuu na wabunge walipata nafasi ya kulijadili suala hilo kwa undani kwamba je tunaanzisha jumuiya ya aina gani?
“Novemba 30 , 1999 ukasainiwa mkataba (Treaty for the Establishment of East African Community) viongozi wakakubaliana kuwa utaanza rasmi kazi zake Julai mosi 2000. mkataba ule umejikita katika mambo makuu matano, kwanza muundo, je tutakuwa na muundo wa aina gani?
Muundo wa Jumuiya:
“Makubaliano yakawa kwamba Jumuiya ya Afrika Mashariki itakuwa na asasi (organs) mbalimbali ambazo zitasaidia kusukuma mbele azma ya jumuiya yenyewe. Hivyo tukakubaliana kwamba kutakuwa na Sekretarieti na Arusha itakuwa ndiyo makao makuu ya jumuiya. Sekretarieti itasimamia shughuli za kila siku za jumuiya, pia tukakubaliana kuwa kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo kazi yake itakuwa ni kusimamia sera. Ilionekana kwamba kazi kubwa ya Jumuiya ni kuainisha na kuziweka sawa sera zetu kwa sababu tutakuwa na sera zinazotofautiana,” anasema Dk. Nangale.
“Asasi ya tatu ni Bunge, kwamba tutakuwa na Bunge la Afrika Mashariki ambalo kazi yake kubwa itakuwa ni kutunga sheria ambazo zitakuwa zinaongoza masuala yote ambayo tutakubalina wkamba tutayafanya kwa pamoja, siyo kutunga sheria zote ila kuhusu yale mambo tuliyokubaliana kwa wakati huo.
“Asasi nyingine ni Mahakama ya Afrika Mashariki. Mahakama hii si mahakama ya rufaa, ni mahakama ambayo kimsingi inatafsiri uhusiano wetu kwa maana ya kutafsiri katiba. Kama kuna tofauti zozote za utekelezaji wa katiba au masuala tuliyokubaliana, mahakama itakuwa inaingilia kati kutoa ufafanuzi na kutoa mapendekezo kwamba hili limefanyika sawa au siyo sawa.
“Asasi nyingine ni ‘Summit,’ Wakuu wa Nchi. Hawa watakutana katika Baraza lao la Wakuu wa Nchi, hawa ndio wasimamizi wakuu wa shughuli zote za Jumuiya. Kazi yao moja ni kuridhia yale tuliyoyapitisha bungeni na ni lazima marais wote waridhie ndipo suala hilo litakapopita. Kwa hiyo Summit ndiyo asasi ya juu zaidi kuliko asasi zote za Afrika Mashariki.”
Misingi ya Ushirikiano (The Principle of Cooperation):
Shabaha yetu ilikuwa ni kutoka kwenye ushirikiano mdogo (Cooperation) kwenda kwenye mahusiano makubwa (Integration). Ili tufanye hivyo kuna misingi mitatu tuliyokubaliana.
Msingi wa kwanza ni ‘Principle of Subsidiarity’;
Ni msingi ambao tunakubaliana kwamba katika ushirikiano wetu hatuwezi tukashirikiana katika kila kitu, kuna baadhi ya mambo tutashirikiana na baadhi ya mambo hatuwezi kushirikiana. Kwa hiyo tutashirikiana katika masuala fulani fulani ambayo tunadhani kwamba tunaweza tukashirikiana kwa ridhaa ya nchi zenyewe.
Msingi wa pili ni ‘Principle of Variable Geometry’;
Ni msingi ambao unatambua kwamba nchi zetu ziko tofauti, kiuchumi, kisiasa, kimuundo na masuala mengi ambayo yako tofauti, kwa hiyo tunakubali kwamba asasi mbalimbali zilizomo ndani ya hizi nchi zitashirikiana kwa sasi zao na utaratibu wao. Kwa mfano jumuiya za wakulima labda zinakwenda taratibu kuliko zile za wafanyabiashara, kwa hivyo zitakwenda kwa kasi tofauti na misingi tofauti.
Msingi wa tatu ni “Principle of Assemetry’
Msingi huu unasema kwamba iwapo A ni sawa na B siyo lazima B iwe sawa na A. Maana yake ni kwamba kwa kutambua tofauti zetu siyo lazima nchi moja inavyoifanyia nchi nyingine kwamba ni lazima nchi hiyo nayo ifanye hivyo hivyo. Kwa mfano msingi huu umefanyiwa kati katika ushirikiano wa forodha, kwamba Tanzania itapeleka bidhaa zake Kenya bila ushuru kwa sasa hivi, wakati Kenya tutawatoza ushuru ili kujipa muda wa kujirekebisha kwa muda wa miaka mitano.
Namna ya kufikia maamuzi:
“Tulikubaliana katika Afrika Mashariki kwamba makubaliano yote yatafikiwa kwa pamoja. Kama limekuja jambo ambalo linataka maamuzi, ni lazima nyote mukubali, yaani nchi zote tatu zikubali. Hivyo tulikubaliana kwamba maamuzi yote ya Afrika Mashariki yatafanywa kwa ‘consesus’ kwa maana ya kwamba, Baraza la Mawaziri likikutana, Wakuu wa nchi wakikutana, kama mmoja atatofautiana na wenzake ina maana kwamba hilo suala litaendelea kujadiliwa, kwa hiyo majadiliano yataendelea mpaka wote wakubaliane, kwa hiyo ukisikia maamuzi yametolewa ya Afrika Mashariki ujue kwamba wote wamekubaliana, hakuna suala la kura bali makubaliano ya pamoja.
Awamu za utekelezaji wa makubaliano:
Tulikubalina kuhusu mahusiano yetu yaendeje, tulikubaliana kwamba tutakwenda hatua kwa hatua. Tulikubaliana kuwa kitu cha kwanza tutakachoanza nacho ni umoja wa ushuru wa forodha (Customs Union). Kwa sababu ilionekana kwamba uhusiano wetu mkubwa ambao ni lazima tuuimarishe ni ule wa kibiashara, ili kuwapa watu wetu masoko na kuinua maisha yao kupitia biashara.
Kwa hivyo tuliamua tuwe na awamu za mashirikiano, tukianzia na Umoja wa Ushuru wa Forodha. Suala la ushuru wa Forodha lilianza kujadiliwa tokea mwaka 1999 hadi 2004, protokali ikasainiwa Machi, 2004 na Bunge tukapitisha sheria ya Ushuru wa Forodha Desemba 2004 na ikaanza kutumika Januari 2005.
Awamu ya pili ni kuanzisha Soko la Pamoja (Common Market), majadiliano yake yameanza Julai mwaka huu na yataendelea mpaka 2008. Soko la pamoja linajumuisha pia masuala ya uhamiaji (free movement of people), masuala ya ajira, masuala ya kufanya biashara kwa pamoja yaani eneo moja la kibiashara duniani (East Africa is a single destination), kuwa na sheria zinazofanana, kuwa na sera zinazofanana hususan zile za kazi, kwamba tukiwa na sheria na sera zinazofanana za kazi, watu wetu wanaweza wakafanya kazi katika hizi nchi bila matatizo, tuwe na pasi za kusafiria za Afrika Mashariki na pia tuwe na vitambulisho.
Awamu ya tatu ni kuwa na Sarafu ya Pamoja (Single Currency/Monetary Union)
Majadiliano yalipangwa yaanze mwaka 2009 hadi 2011, hapo ndipo tuwe na Sarafu moja. Mwisho kabisa, baada ya kupitia awamu zote hizo ndipo tutakwenda kwenye Ushirikiano wa Kisiasa (Political Federation).
Mkataba uliposainiwa mwaka 1999 kulikuwa kuna makubaliano kwamba Afrika Mashariki itakwenda kwa awamu mpaka kufikia Federation, haikupangwa ratiba ya Federation kwa wakati huo, tulikubaliana kwamba tukimaliza awamu moja tutakwenda nyingine. Kwa mfano Ushuru wa Pamoja wa Forodha ilikuwa ni awamu ambayo ilipaswa kufanyiwa kazi kwa miaka mitano toka 2005 hadi 2010. Halafu majadiliano ya Soko la Pamoja yanaanza, na labda itaanza kufanya kazi mwaka 2009 hadi miaka mitano, baada ya hapo Sarafu ya Pamoja, majadiliano yanaweza yakaanza mapema lakini utekelezaji wake ukafanywa baadaye. Baada ya hapo ndio tuingie katika Shirikisho la Kisiasa.
Jumuiya ya watu
Makubaliano yaliyofikiwa mwaka 1999 katika kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki tulikubaliana kuwa tuunde jumuiya ya watu. Jumuiya ya mwanzo iliyovunjika ilikuwa ni ya Serikali (more inter-governmental). Sasa hii tunataka iwe ya watu (people centered), kwa hiyo watu washirikiane katika hatua mbalimbali na asasi mbalimbali. Pamoja na kuwa Serikali ni wadau lakini hata sisi wananchi pia ni wadau. Kwa hivyo hata sekta binafsi na asasi za kijamii zitapewa nafasi katika Jumuiya hii mpya ya Afrika Mashariki.
Kwanini haraka ya kwenda kwenye ushirikiano wa kisiasa?
“Miaka miwili iliyopita Rais Benjamin Mkapa, Rais Museveni na Rais Mwai Kibaki walikutana Nairobi katika mkutano wa dharura. Kulikuwa kuna ajenda kwamba kwani ni lazima awamu zilizopangwa kufikia Ushirikiano ni lazima ziende kwa utaratibu huo? Haiwezekani kuziharakisha? Wakaunda Tume kujadili suala hilo, wakaunda Tume ya Wako ambayo ilizunguka na kukutana na wadau mablimbali, wabunge, wananchi, wafanyabiashara na ilifanya kazi kwa muda wa miezi sita. Ilipotoa ripoti yake, ile Tume ikasema kwamba wananchi wa Afrika Mashariki wako tayari kuharakisha muungano wa Afrika Mashariki na ikatengeneza ratiba kwamba ifikapo mwaka 2010 tuwe tumeshafikia hatua fulani, 2012 tuwe na kura ya maoni na 2013 hizi nchi ziwe zimeshaungana kisiasa,” anasema Dk. Nangale.
“Hiyo haina maana kwamba hatua za kufikia Ushirikiano wa kisiasa zitafutwa, la hasha, bali awamu zote zitaharakishwa ama zitatekelezwa kwa pamoja.
Ripoti ile ikapelekwa kwenye mabunge ikajadiliwa. Bunge la Uganda waliizungumza, Bunge la Kenya wabunge walisomewa tu lakini hawakuizungumza rasmi, Bunge la Tanzania haikuizunguza rasmi ripoti ile. Katika Bunge la Tanzania ripoti ile ilizungumzwa kwenye semina ya wabunge, wabunge wengi waliikataa ripoti ile, lakini haikuzungumzwa katika kikao rasmi cha Bunge.
Katika Bunge la Afrika Mashariki ripoti ile ilipelekwa ingawa haikujadiliwa rasmi. Wakuu wa nchi walipopata ile ripoti wakakubaliana kuunda kamati za kuendesha mijadala, ili wananchi wapate nafasi ya kutoa maoni. Kila nchi ikaunda kamati, kamati hizo zimepewa miezi minane ya kukusanya maoni ya wananchi. Itakapofika Mei mwakani wanapaswa kuiwasilisha ripoti yao kwenye Baraza la mawaziri.
Lakini cha ajabu ni kwamba kwa upande wa Tanzania ndio kwanza inajiweka sawa katika kazi ya kukusanya maoni? Imesalia miezi minne tu Kamati hiyo inapaswa iwasilishe ripoti yake.
Friday, January 19, 2007
samahanini ndugu zangu
Hi Comrades.
Naomba mnisamehe kwa kutoshiriki katika uwanja huu adhimu kwa siku nyingi, siyo kama sipendi au siwezi kuiba muda kidogo ili ku-share nanyi some important issues but because nilisahau password kutokana na kuwa na mazonge mengi, ikawa kila nikijaribu kuomba administration wanisaidie kukumbuka password yangu, inashindikana.
Ahsanteni nyote mliokuwa mkiniandikia kuniuliza kulikoni na samahanini wote niliowadodesha halafu nikawakatishia bila kumaliza kiu.
Sasa nimerudi nikiwa na ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.
Nawatakia wote heri ya mwaka mpya 2007.
May your happiness increase like fuel price in Tanzania,
And your worries fall like number of votes to the opposition block in Tanzania,
So that your desires bu fulfilled massively like Kikwete's trips abroad.
May your problems vanish like TANESCO's electricity.
I wish u a Happy and Prosperous year - 2007.
Naomba mnisamehe kwa kutoshiriki katika uwanja huu adhimu kwa siku nyingi, siyo kama sipendi au siwezi kuiba muda kidogo ili ku-share nanyi some important issues but because nilisahau password kutokana na kuwa na mazonge mengi, ikawa kila nikijaribu kuomba administration wanisaidie kukumbuka password yangu, inashindikana.
Ahsanteni nyote mliokuwa mkiniandikia kuniuliza kulikoni na samahanini wote niliowadodesha halafu nikawakatishia bila kumaliza kiu.
Sasa nimerudi nikiwa na ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.
Nawatakia wote heri ya mwaka mpya 2007.
May your happiness increase like fuel price in Tanzania,
And your worries fall like number of votes to the opposition block in Tanzania,
So that your desires bu fulfilled massively like Kikwete's trips abroad.
May your problems vanish like TANESCO's electricity.
I wish u a Happy and Prosperous year - 2007.
Subscribe to:
Posts (Atom)